Pages

Monday, October 7, 2013

MWAMBA

Biblia (tafsiri ya King James) inaonyesha kuwa neno mwamba limeandikwa mara 142 katika mistari 128! Kwangu hii takwimu ni ya ajabu kwa sababu katika baadhi ya hii mistari neno mwamba limeonekana zaidi ya mara moja!

Unaposoma Zaburi unagundua kwamba mwimba-zaburi mara nyingi anamtambua Mungu kama Mwamba. Hapa kuna siri ya ajabu sana. Unapomtambua Mungu kama mwamba wako, unakuwa umemfanya Mungu kuwa kila kitu kwako. Unamwambia kuwa Yeye ni kila kitu kwako na bila Yeye huwezi kufanya lolote. Kwa kumwita yeye Mwamba wako, unamwambia:

Wewe ni nyumba yangu
Wewe ni makazi yangu
Wewe ni usalama wangu
Wewe ni tegemeo langu
Wewe ni kimbilio langu
Wewe ni maficho yangu
Wewe ni pumziko langu
Wewe ni muziki wangu
Wewe ni mgahawa wangu
Wewe ni ngome yangu
Wewe ni kinga yangu
Wewe ni nguvu yangu
Wewe ni udongo wangu na kwako nitakita mizizi. Orodha hii ni “Endless

And he (David) said, The LORD is my rock, my fortress and my deliverer; my God is my rock, in whom I take refuge: my shield, and the horn of my salvation. He is my stronghold, my refuge and my saviour – from violent men you save me (2 Samuel 22:23, NIV, emphasis mine).



Discover Yahoo!
Have fun online with music videos, cool games, IM & more. Check it out!

DISAPOINTED? HERE IS A SOLUTION!

Failure in life is one of disappointment event that no one would like to meet. When we fail, we become like a patient admitted in the hospital; we need confort, some one to be closer to you, love and care.

The opposite comes true to many people when another person fail. It is like the story in the book 'ONLY FOOLS DIE'. In that book the author argue that, for any  dealth there is a foolis reason reason that a died person is associated with, for example, a malaria died person may be associated with lazziness, "Why did they delay to take him to the hospital?" one may say;  in a car accident you may hear "The driver was so fast, but the passengers were just silent or shouting, 'speed up we are late'"  This is how always people act.

Athough we hate failures, but we always meet some failure in life. Failing in one area does not prove disability in other areas of life, that may be a mechanism that enhance specialization in the society. I do not support failing, but the fact remain the same tha we sometimes fail and but also forget ourselves when we see  others failing in areas that we  are successiful, for example in academics, when a student fail many people say  he was so lazzy, he/she  involved in  extra curricullum activities other tahn academics. The reason given may be true, but should we react that way? On the other side we may misjugde failed fellows because failing in an exam may be a function of some psychologica, physiologica, bological and /or sociological changes just few minutes before commencing the examonations. Actually, judging the failed as lazzy is like the statement one given in the title of the book ONLY FOOLS DIE.

All in all, the fact remain, we become successiful not because we can be so, but because of God's mercies. A failed person needs love. comfort, closeness just like a patient in the hospital. Lets help the needy in times of truble and not adding more trouble to them by blaming their weaknesses. Even if they have weakenesses associated with their failure, are you perfect to stone them?

'A friend in need is a friend indeed' and Dini iliyo nzuri ni kuwasaidia wajane na yatima, wenye shida na taabu. Pray for all in trials, troubles and disappointments. This perfect our life in Jesus. When you face a faile person, ACT, do not REACT

Saturday, October 5, 2013

FAITH

Many have said of faith, but what is it for sure?
FAITH IS:
  1. An expression of confidence in God (Heb 10:35-36)
  2. Is an act motivated by The Word of God (James 2:18)
  3. It is a Translating Force from invisible to visible  (Eph 2:8-9)
  4. IsObeying God to receive waht He has promised in our lives
  5. Is behaving in God's Word
  6. Is reasoning with God on issues in order to get proper answers
  7. I seeing things the way God see them
  8. Is power point of Christian life as it connect man to the power of God
  9. Is a weapon of war. when in trouble, your faith tell you stand stii for there is salvation of God before you
  10. Is the knowledge of God's power in man's life

Saturday, September 7, 2013

JE, UTAMFUNIKA NUHU?




 TAZAMA
Mwanzo sura 6-9 inazungumza kuhusu mtumishi wa Mungu Nuhu ambaye Mungu alimmwamuru kutengeneza Safina ili kukisaza kizazi toka mafuriko ambayo aliyakusudia kwa wanadamu waliomwasi. Huyu ni mtumishi ambaye Mungu alimtumia kwa jinsi ya tofauti sana.

Baadaye tunaona akiwa katika udhaifu:
Mwanzo 9:20-21
Ø  Hapa mtumishi wa Mungu amelewa mvinyo hadi kuwa uchi katika hema yake.
Mwanzo 9:22-23
Ø  Ham aliona uchi wa baba yake yake akaenda kuwaambia kaka zake nje
Ø  Lakini, Shem na Japhet walichukua nguo na kumfunika baba yao; hawakumwangalia uchi wake.

TUNACHOJIFUNZA
1.   Mungu anaweza kuruhusu kuona madhaifu ya wenzetu akitaka kuona mwitikio wetu.
2.   Baadhi yetu hufurahia kutangaza udhaifu wa ndugu zao (hata wakati mwingine Baba yao –Mchungaji-) kama ilivyokuwa kwa Ham
3.   Wengi wetu tunapoona mwezetu maefanya kosa/dhambi; hufurahia na kuanza kutangaza, wakati mwingine k=hata kwa kusema, ‘Nilijua hajaokoka’  au ‘alijikuwa kimbelembele, nilijua hafiki mbali’.
4.   Watu wa Mungu (kama ilivyokuwa kwa Shem na Japhet), hutoa msaada kwani ‘upendo husitiri wingi wa dhambi’.
5.   Yesu angeangalia udhaifu wetu kwa jicho tunaloangalia udhaifu wa wenzetu, asingekuja ulimwenguni. Lakini, yesu huangalia udhaifu wetu kwa jicho la upendo ili kwa upendo huo tunabadilika. (Mithali 10:12 – ‘upendo husitiri wingi wa dhambi’)

Matokeo
Nuhu alimlaani Ham na laana hiyo ilikifuata kizazi chake cha Wakaanani. Unapohukumu/ kutangaza mudhaifu wa wenzako, roho hiyo inakufuata na itakuangamiza.

Swali Muhimu
Unaitikiaje unapomkuta mwenzako ametenda kosa? Unaposikia jambo lisilo zuri kuhusu ndugu yako, unafanya nini?
Je, utakuwa msambazaji wa maneno mabaya ukidhani ni sifa njema;
au
Utamwombea na kumshauri
Hizi ni nguvu mbili zinazofanya kazi kanisani siku hizi, moja inaishia kwenye maangamizi ya kiroho na nyingine kwenye ukombozi na kuimarisha kanisa. Uchaguzi ni wako.
Swali linabaki, Je utamfunika Nuhu? 

MAISHA MAPYA YA WOKOVU





MPANGO WA WOKOVU
1. Mungu anakupenda na ana mpango mzuri kwa maisha yako Yohana 3:16, 10:10b
2. Mwanadamu ametenda dhanbi na kutengwa na Mungu Warumi 3:23, 6:23, Waefeso 2:8-9
3. Yesu Kristo pekee ndie mwokozi wetu. Alikufa kwaajili yetu na akafufuka tupate uzima Warumi 5:8, Yohana 14:6, 1wakorintho 15:3-6
4. Lazima kumpokea Yesu kama mwokozi Yohana 1:12, Ufunuo 3:20, Warumi 10:9

KUUNGAMA DHAMBI
Si mpango wa Mungu utende dhambi. Lakini, kama wanadamu, tunakumbana na majaribu. Hii ina maana kuwa, bado tunapambana na dhambi maishani mwetu. Kinachotokea unapotenda dhambi si kupoteza wokovu wako, bali ushirka wako na Mungu uaathirika. Kama baba wa upendo, Mungu ametoa njia ya kushinda majaribu, na kumrudia tunapotenda dhambi. Biblia inasema ‘Kama tukisema hatuna dhambi twajidanganya wenyewe, na kweli haimo ndani yetu. Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu zote na kutusafisha na uovu wetu wote’ (1Yohana 1:8-9)

Kuungama dhambi si kusema tu ‘nimefanya dhambi’. Ungamo la kweli linataka:
1.     Uwe mkweli. Tambua dhambi/kosa ulilotenda
2.     Tubu dhambi kwa Mungu (ukimaanishaa kuziacha dhambi nakutotenda dhambi tena) Zaburi 32:5
3.     Uwe wazi (mwambie Mungu hakika ulichotenda)
4.     Uwe haraka kutambua kosa lako. Mara unapogundua kuwa umetenda dhambi, ungama. Kama si hivyo upo katika hatari ya kuanguka katika dhambi nyingine zaidi.
5.     Uwe mnyenyekevu kwa kuomba msamaha kwa wote walioathioriwa na dhambi yako Yakobo 5:16, Mathayo 5: 23-24, 1Yohana 5:20
6.     Kubali msamaha. Hautakiwi kuendelea kutubia dhambi ambayo umeshatubia kana kwamba Mungu hasamehe makosa. Kama Mungu ametusamehe, ni muhimu kukubali msamaha huu, na kuamini, na kumshukuru. Kataa mashtaka ya shetani kwamga haukusamehewa/ au hauwezi kusamehewa.

KAMA UMEOKOKA JUA SASA WEWE:-
1.     Ni kiumbe kipya (2Wakorintho 5:17)
2.     Ni mwana wa Mungu (Yohana 1:12, Warumi 8:14-15, Wagalatia 3:26, 4:6)
3.     Umekombolewa na kusamehewa dhambi zako zote (Wakolosai 1:14)
4.     Umewekwa huru kabisa, mbali na hukumu na nguvu ya dhambi ( Warumi 8:1; 6:1-6)
5.     Unayo haki bila aibu kukisogelea kiti cha enzi cha Mungu kuomba neema nyakati za mahitaji (Waebrania 4:16)
6.     Una haki katika Kristo, umesamehewa dhambi zote (Warumi 5:1)
7.     Ni mtumwa wa haki (Warumi 6:18)
8.     Ni mtakatifu (Waefeso 1:1, Wakorintho 1:2, Wafilipi 1:1)
9.     Ni chumvi na nuru ya ulimwengu (Mathayo 5:13-14)
10.  Ni rafiki na chaguo la Yesu Kristo kumzalia matunda (Yohana 15:15-16)
11.  Ni mtumishi wa mungu (Warumi 6:22, Waefeso 3:1; 4:1)
12.  Ni hekalu takatifu, mahali ambapo Mungu Roho Mtakatifu anakaa (1Wakorintho 3:16,; 6:19)
13.  Umenunuliwa kwa gharama kubwa, Damu ya Yesu, na hivyo ni mali ya Mungu, unaishi kwaajili ya Kristo (1Wakorintho 6:19-20, 2Wakorintho 5:14-15)
14.  Ni kiungo katika mwili wa Kristo (1Wakorintho 12:27, Waefeso 5:30)
15.  Umepatanishwa na Mungu kwa njia ya Yesu, hivyo ni mpatanishi (2Wakorintho 5:18-19)
16.  Ulisulubiwa pamoja na Kristo, si wewei unayeishi, ni Kristo ndani yako (Wagalatia 2:20)
17.  Ulichaguliwa na Kristo kabla ya kuwekwa misiingi ya ulimwengu kuwa mtakatifu bila ya mawaa mbele zake (Waefeso 1:4)
18.  Ni mrithi katika ufalme wa Mungu, kwa sababu ni mtoto wake (Wagalatia 4:6-7)
19.  Ni mtendakazi wa Mungu, uliyezaliwa mara ya pili (uliyeokoka) ili kufanya kazi yake (Waefeso 2:10)
20.  Ni mtakarifu na mwenye haki wa Mungu (Waefeso 4:24)
21.  Ni raia wa mbinguni (Wafilipi 3:20, Waefeso 2:6)
22.  Ni msafiri katika dunia hii, ambayo unishi kwa muda tu (1Petro 2:11)
23.  Ni aliyekombolewa toka utawala wa shtani na kupelekwa kwenye ufalme wa mungu (Wakolosai 1:13)
24.  Ni adui wa shetani (1Petro5:8)
25.  Ni mzaliwa wa Mungu. Shetani hana mamlaka kukukugusa (1Yohana 5:18; Kristo mwenyewe anaishi ndani yako (Wakolosai 1:13)
26.  Umezaliwa na Mungu, mtakatifu na mpendwa (Wakolosai 3:12; Wathesalonike 1:4)
27.  Umepewa ahadi kuwa mno toka kwa Mungu (2Petro 1:4)
28.  Utakua kama Kristo atakaporudi mara ya pili (1Yohana 3:1-2)
29.  Kwa neema ya Mungu upo kama hivyo ulivyo (1Wakorintho 15:10)

JINSI YA KUTEMBEA NA YESU
1.     Soma Biblia kila siku ili umjue yesu vema
2.     Zungumza na Mungu kila siku kwa njia ya maombi
3.     Ruhusu Mungu atawale maisha yako, ukijitoa kwa mapenzi yake
4.     Zungumza na wengine kuhusu yesu
5.     Shirikiana na wengine katika ushirika/ibada mahali Yesu anahubiriwa
6.     Jiunge na mshirika mmoja au wawili ambao mnaweza kuomba pamoja na kushirikiana mafanikio na matatizo yako
7.     Onyesha maisha yako mapya kupitia upendo na kuwajali wengine

JINSI YA KUISHI MAISHA YA WOKOVU KILA SIKU
1. Andaa moyo wako: Jichunguze, Ungama dhambi, Omba ufahamu Zaburi 5:3; 139:23-24; 51:10, Waebrania 4:16
2. Jifunze biblia. Kila unaposoba Biblia andika neno lililokusa sana, wazo kuu na maana ya neno katika maisha yako. Jiulize kama kuna amri au mfano wa kufuata, dhambi ya kutubia na ahadi ya Mungu kwako
3. Omba: Ongea na Mungu kuhusu neno ulilosona, mwabudu na kumsifuMungu kwa ukuu wake, na mpe Mungu mahitaji yako
4. Mwimbie Mungu wimbo wa sifa au tenzi. Wimbo wa kuabudu,  wa taratibu na muziki mwororo utasaidia kukusogeza karibu na Mungu na kumsifu Yeye
5. Omba kujazwa na Roho Mtakatifu. Omba maombi ya kujitoa mbele za Mungu, mfano; ‘Baba katika Jina la Yesu,        
Najitoa mbele zako,
Niwe chombo kikufaacho,
Tawala akili zangu na kila ninachofikiri,
Tawala macho yangu na kila ninachotazama,
Tawala masikio yangu na kila ninachosikia,
Tawala ulimi wangu na kila ninachonena,
Tawala moyo wangu na tabia zangu,
Tawala mikono yangu na yote nifanyayo,            
Tawala miguu yangu na pote niendapo,
Tawala mwili wangu ni hekalu lako Bwana,
 Nijaze na Roho Mtakatifu,
 Nataka kukutii, Nataka kukufuata wewe
Siku zote za maisha yangu, Nisaidie Bwana, Haleluya! Sante Yesu!

6. Fanyia kazi yale uliyojifunza
7. Kariri mstari mmoja, uandike katika daftari.

KARIBU KTK MAISHA MAPYA