Pages

Saturday, September 7, 2013

JE, UTAMFUNIKA NUHU?




 TAZAMA
Mwanzo sura 6-9 inazungumza kuhusu mtumishi wa Mungu Nuhu ambaye Mungu alimmwamuru kutengeneza Safina ili kukisaza kizazi toka mafuriko ambayo aliyakusudia kwa wanadamu waliomwasi. Huyu ni mtumishi ambaye Mungu alimtumia kwa jinsi ya tofauti sana.

Baadaye tunaona akiwa katika udhaifu:
Mwanzo 9:20-21
Ø  Hapa mtumishi wa Mungu amelewa mvinyo hadi kuwa uchi katika hema yake.
Mwanzo 9:22-23
Ø  Ham aliona uchi wa baba yake yake akaenda kuwaambia kaka zake nje
Ø  Lakini, Shem na Japhet walichukua nguo na kumfunika baba yao; hawakumwangalia uchi wake.

TUNACHOJIFUNZA
1.   Mungu anaweza kuruhusu kuona madhaifu ya wenzetu akitaka kuona mwitikio wetu.
2.   Baadhi yetu hufurahia kutangaza udhaifu wa ndugu zao (hata wakati mwingine Baba yao –Mchungaji-) kama ilivyokuwa kwa Ham
3.   Wengi wetu tunapoona mwezetu maefanya kosa/dhambi; hufurahia na kuanza kutangaza, wakati mwingine k=hata kwa kusema, ‘Nilijua hajaokoka’  au ‘alijikuwa kimbelembele, nilijua hafiki mbali’.
4.   Watu wa Mungu (kama ilivyokuwa kwa Shem na Japhet), hutoa msaada kwani ‘upendo husitiri wingi wa dhambi’.
5.   Yesu angeangalia udhaifu wetu kwa jicho tunaloangalia udhaifu wa wenzetu, asingekuja ulimwenguni. Lakini, yesu huangalia udhaifu wetu kwa jicho la upendo ili kwa upendo huo tunabadilika. (Mithali 10:12 – ‘upendo husitiri wingi wa dhambi’)

Matokeo
Nuhu alimlaani Ham na laana hiyo ilikifuata kizazi chake cha Wakaanani. Unapohukumu/ kutangaza mudhaifu wa wenzako, roho hiyo inakufuata na itakuangamiza.

Swali Muhimu
Unaitikiaje unapomkuta mwenzako ametenda kosa? Unaposikia jambo lisilo zuri kuhusu ndugu yako, unafanya nini?
Je, utakuwa msambazaji wa maneno mabaya ukidhani ni sifa njema;
au
Utamwombea na kumshauri
Hizi ni nguvu mbili zinazofanya kazi kanisani siku hizi, moja inaishia kwenye maangamizi ya kiroho na nyingine kwenye ukombozi na kuimarisha kanisa. Uchaguzi ni wako.
Swali linabaki, Je utamfunika Nuhu? 

No comments: