TAZAMA
Mwanzo sura 6-9 inazungumza kuhusu mtumishi
wa Mungu Nuhu ambaye Mungu alimmwamuru kutengeneza Safina ili kukisaza kizazi
toka mafuriko ambayo aliyakusudia kwa wanadamu waliomwasi. Huyu ni mtumishi
ambaye Mungu alimtumia kwa jinsi ya tofauti sana.
Baadaye tunaona akiwa katika udhaifu:
Mwanzo 9:20-21
Ø Hapa
mtumishi wa Mungu amelewa mvinyo hadi kuwa uchi katika hema yake.
Mwanzo 9:22-23
Ø Ham
aliona uchi wa baba yake yake akaenda kuwaambia kaka zake nje
Ø Lakini,
Shem na Japhet walichukua nguo na kumfunika baba yao; hawakumwangalia uchi wake.
TUNACHOJIFUNZA
1.
Mungu
anaweza kuruhusu kuona madhaifu ya wenzetu akitaka kuona mwitikio wetu.
2.
Baadhi
yetu hufurahia kutangaza udhaifu wa ndugu zao (hata wakati mwingine Baba yao –Mchungaji-) kama ilivyokuwa kwa Ham
3.
Wengi wetu tunapoona mwezetu maefanya
kosa/dhambi; hufurahia na kuanza kutangaza, wakati mwingine k=hata kwa kusema, ‘Nilijua hajaokoka’ au ‘alijikuwa
kimbelembele, nilijua hafiki mbali’.
4.
Watu wa Mungu (kama
ilivyokuwa kwa Shem na Japhet), hutoa msaada kwani ‘upendo husitiri wingi wa
dhambi’.
5.
Yesu angeangalia udhaifu wetu kwa jicho
tunaloangalia udhaifu wa wenzetu, asingekuja ulimwenguni. Lakini, yesu
huangalia udhaifu wetu kwa jicho la upendo ili kwa upendo huo tunabadilika.
(Mithali 10:12 – ‘upendo husitiri wingi wa dhambi’)
Matokeo
Nuhu alimlaani Ham na laana hiyo ilikifuata
kizazi chake cha Wakaanani. Unapohukumu/ kutangaza mudhaifu wa wenzako, roho
hiyo inakufuata na itakuangamiza.
Swali
Muhimu
Unaitikiaje unapomkuta mwenzako ametenda
kosa? Unaposikia jambo lisilo zuri kuhusu ndugu yako, unafanya nini?
Je,
utakuwa msambazaji wa maneno mabaya ukidhani ni sifa njema;
au
Utamwombea
na kumshauri
Hizi ni nguvu mbili zinazofanya kazi
kanisani siku hizi, moja inaishia kwenye maangamizi ya kiroho na nyingine
kwenye ukombozi na kuimarisha kanisa. Uchaguzi ni wako.
Swali linabaki, Je utamfunika Nuhu?
No comments:
Post a Comment