Pages

Saturday, September 7, 2013

MAISHA MAPYA YA WOKOVU





MPANGO WA WOKOVU
1. Mungu anakupenda na ana mpango mzuri kwa maisha yako Yohana 3:16, 10:10b
2. Mwanadamu ametenda dhanbi na kutengwa na Mungu Warumi 3:23, 6:23, Waefeso 2:8-9
3. Yesu Kristo pekee ndie mwokozi wetu. Alikufa kwaajili yetu na akafufuka tupate uzima Warumi 5:8, Yohana 14:6, 1wakorintho 15:3-6
4. Lazima kumpokea Yesu kama mwokozi Yohana 1:12, Ufunuo 3:20, Warumi 10:9

KUUNGAMA DHAMBI
Si mpango wa Mungu utende dhambi. Lakini, kama wanadamu, tunakumbana na majaribu. Hii ina maana kuwa, bado tunapambana na dhambi maishani mwetu. Kinachotokea unapotenda dhambi si kupoteza wokovu wako, bali ushirka wako na Mungu uaathirika. Kama baba wa upendo, Mungu ametoa njia ya kushinda majaribu, na kumrudia tunapotenda dhambi. Biblia inasema ‘Kama tukisema hatuna dhambi twajidanganya wenyewe, na kweli haimo ndani yetu. Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki, atatusamehe dhambi zetu zote na kutusafisha na uovu wetu wote’ (1Yohana 1:8-9)

Kuungama dhambi si kusema tu ‘nimefanya dhambi’. Ungamo la kweli linataka:
1.     Uwe mkweli. Tambua dhambi/kosa ulilotenda
2.     Tubu dhambi kwa Mungu (ukimaanishaa kuziacha dhambi nakutotenda dhambi tena) Zaburi 32:5
3.     Uwe wazi (mwambie Mungu hakika ulichotenda)
4.     Uwe haraka kutambua kosa lako. Mara unapogundua kuwa umetenda dhambi, ungama. Kama si hivyo upo katika hatari ya kuanguka katika dhambi nyingine zaidi.
5.     Uwe mnyenyekevu kwa kuomba msamaha kwa wote walioathioriwa na dhambi yako Yakobo 5:16, Mathayo 5: 23-24, 1Yohana 5:20
6.     Kubali msamaha. Hautakiwi kuendelea kutubia dhambi ambayo umeshatubia kana kwamba Mungu hasamehe makosa. Kama Mungu ametusamehe, ni muhimu kukubali msamaha huu, na kuamini, na kumshukuru. Kataa mashtaka ya shetani kwamga haukusamehewa/ au hauwezi kusamehewa.

KAMA UMEOKOKA JUA SASA WEWE:-
1.     Ni kiumbe kipya (2Wakorintho 5:17)
2.     Ni mwana wa Mungu (Yohana 1:12, Warumi 8:14-15, Wagalatia 3:26, 4:6)
3.     Umekombolewa na kusamehewa dhambi zako zote (Wakolosai 1:14)
4.     Umewekwa huru kabisa, mbali na hukumu na nguvu ya dhambi ( Warumi 8:1; 6:1-6)
5.     Unayo haki bila aibu kukisogelea kiti cha enzi cha Mungu kuomba neema nyakati za mahitaji (Waebrania 4:16)
6.     Una haki katika Kristo, umesamehewa dhambi zote (Warumi 5:1)
7.     Ni mtumwa wa haki (Warumi 6:18)
8.     Ni mtakatifu (Waefeso 1:1, Wakorintho 1:2, Wafilipi 1:1)
9.     Ni chumvi na nuru ya ulimwengu (Mathayo 5:13-14)
10.  Ni rafiki na chaguo la Yesu Kristo kumzalia matunda (Yohana 15:15-16)
11.  Ni mtumishi wa mungu (Warumi 6:22, Waefeso 3:1; 4:1)
12.  Ni hekalu takatifu, mahali ambapo Mungu Roho Mtakatifu anakaa (1Wakorintho 3:16,; 6:19)
13.  Umenunuliwa kwa gharama kubwa, Damu ya Yesu, na hivyo ni mali ya Mungu, unaishi kwaajili ya Kristo (1Wakorintho 6:19-20, 2Wakorintho 5:14-15)
14.  Ni kiungo katika mwili wa Kristo (1Wakorintho 12:27, Waefeso 5:30)
15.  Umepatanishwa na Mungu kwa njia ya Yesu, hivyo ni mpatanishi (2Wakorintho 5:18-19)
16.  Ulisulubiwa pamoja na Kristo, si wewei unayeishi, ni Kristo ndani yako (Wagalatia 2:20)
17.  Ulichaguliwa na Kristo kabla ya kuwekwa misiingi ya ulimwengu kuwa mtakatifu bila ya mawaa mbele zake (Waefeso 1:4)
18.  Ni mrithi katika ufalme wa Mungu, kwa sababu ni mtoto wake (Wagalatia 4:6-7)
19.  Ni mtendakazi wa Mungu, uliyezaliwa mara ya pili (uliyeokoka) ili kufanya kazi yake (Waefeso 2:10)
20.  Ni mtakarifu na mwenye haki wa Mungu (Waefeso 4:24)
21.  Ni raia wa mbinguni (Wafilipi 3:20, Waefeso 2:6)
22.  Ni msafiri katika dunia hii, ambayo unishi kwa muda tu (1Petro 2:11)
23.  Ni aliyekombolewa toka utawala wa shtani na kupelekwa kwenye ufalme wa mungu (Wakolosai 1:13)
24.  Ni adui wa shetani (1Petro5:8)
25.  Ni mzaliwa wa Mungu. Shetani hana mamlaka kukukugusa (1Yohana 5:18; Kristo mwenyewe anaishi ndani yako (Wakolosai 1:13)
26.  Umezaliwa na Mungu, mtakatifu na mpendwa (Wakolosai 3:12; Wathesalonike 1:4)
27.  Umepewa ahadi kuwa mno toka kwa Mungu (2Petro 1:4)
28.  Utakua kama Kristo atakaporudi mara ya pili (1Yohana 3:1-2)
29.  Kwa neema ya Mungu upo kama hivyo ulivyo (1Wakorintho 15:10)

JINSI YA KUTEMBEA NA YESU
1.     Soma Biblia kila siku ili umjue yesu vema
2.     Zungumza na Mungu kila siku kwa njia ya maombi
3.     Ruhusu Mungu atawale maisha yako, ukijitoa kwa mapenzi yake
4.     Zungumza na wengine kuhusu yesu
5.     Shirikiana na wengine katika ushirika/ibada mahali Yesu anahubiriwa
6.     Jiunge na mshirika mmoja au wawili ambao mnaweza kuomba pamoja na kushirikiana mafanikio na matatizo yako
7.     Onyesha maisha yako mapya kupitia upendo na kuwajali wengine

JINSI YA KUISHI MAISHA YA WOKOVU KILA SIKU
1. Andaa moyo wako: Jichunguze, Ungama dhambi, Omba ufahamu Zaburi 5:3; 139:23-24; 51:10, Waebrania 4:16
2. Jifunze biblia. Kila unaposoba Biblia andika neno lililokusa sana, wazo kuu na maana ya neno katika maisha yako. Jiulize kama kuna amri au mfano wa kufuata, dhambi ya kutubia na ahadi ya Mungu kwako
3. Omba: Ongea na Mungu kuhusu neno ulilosona, mwabudu na kumsifuMungu kwa ukuu wake, na mpe Mungu mahitaji yako
4. Mwimbie Mungu wimbo wa sifa au tenzi. Wimbo wa kuabudu,  wa taratibu na muziki mwororo utasaidia kukusogeza karibu na Mungu na kumsifu Yeye
5. Omba kujazwa na Roho Mtakatifu. Omba maombi ya kujitoa mbele za Mungu, mfano; ‘Baba katika Jina la Yesu,        
Najitoa mbele zako,
Niwe chombo kikufaacho,
Tawala akili zangu na kila ninachofikiri,
Tawala macho yangu na kila ninachotazama,
Tawala masikio yangu na kila ninachosikia,
Tawala ulimi wangu na kila ninachonena,
Tawala moyo wangu na tabia zangu,
Tawala mikono yangu na yote nifanyayo,            
Tawala miguu yangu na pote niendapo,
Tawala mwili wangu ni hekalu lako Bwana,
 Nijaze na Roho Mtakatifu,
 Nataka kukutii, Nataka kukufuata wewe
Siku zote za maisha yangu, Nisaidie Bwana, Haleluya! Sante Yesu!

6. Fanyia kazi yale uliyojifunza
7. Kariri mstari mmoja, uandike katika daftari.

KARIBU KTK MAISHA MAPYA

No comments: