Pages

Thursday, August 29, 2013

ASKOFU MOSES KULOLA AFARIKI DUNIA

habari tulizozipata hivi punde ambazo pia zimethibitishwa na wanafamilia ya Askofu Dk Moses Kulola ni kwamba, askofu huyo wa kanisa la E A G T Ametangulia kwa Bwana leo hii.

Katika mitandao ya kijamii, wengi wametoa maoni yao kuhusu kifo cha Moses Kulola

 Askofu Kulola ni 'Mtumishi wa Mungu mwenye moyo wa Uinjilisti, Aliyefanya kazi kwa muda mrefu tena kwa UAMINIFU MKUBWA, akizunguka huku na kule Tanzania na nchi zingine akibeba habari njema na nzito za Injili ...aliyekubali mateso kwa ajili ya Injili....aliyezaa matunda mengi kiroho....Ninayemheshimu sana ....hata nilipokuwa mdogo niliwahi kuota kuhusu yeye....alihusisha mambo mengi na Injili ....hata watu waliookoka chini yake aliwaita wana wa Injili...Binafsi Yesu alikuwa Rafiki wa pekee kwake....hata cheo cha U dokta hakitoshi kwake ...bado amekuwa mnyenyekevu wa moyo, mwenye huruma sana kwa wanaoteseka ....mkali sana kwa mapepo na nguvu za giza...aiyeogopa kukemea Injili za aina nyingine zinazotaka kutoka kwenye msingi wa injili halisi....Ninamependa sana sana ....sasa ni nini hiki naanza kusikia watu wanasema' (Abel Orgenes) 

'Naomba Isiwe Kweli ..... Vita Amevipiga, Imani Ameilinda na Mwendo ameumaliza.....' (Samwel Sasali) 

'R. I. P. lev moses kolola pumzika kwa amani baba yetu wa kiloho.nipengo kubwa kwa watanzania'  (Ballack Alberto) 



Wengi wametoa masikitiko yao, lakini cha muhimu ni kwamba AMEMTUMIKIA MUNGU KWA UAMINIFU WOTE, tunaamini kuwa amepumzika ba siku ya Mwisho tutamlaki Yesu Kristo pamoja mawinguni tusipozimia mioyo.

BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE
AMEN 

No comments: